Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 17:03

Umoja wa Mataifa wapitisha azimio la kuitaka Russia kuondoa wanajeshi wake Ukraine


Kikao cha Baraza la usalama la UN kuhusu mzozo wa Ukraine, Februari 8, 2023.
Kikao cha Baraza la usalama la UN kuhusu mzozo wa Ukraine, Februari 8, 2023.

Umoja wa Mataifa Alhamisi umeitenga Russia kwa kura nyingi, wakati ikiadhimishwa mwaka mmoja tangu Moscow iivamie Ukraine kwa kutoa wito wa kuwepo kwa amani ya haki na ya kudumu, na kuitaka kwa mara nyingine Moscow kuondoa wanajeshi wake na kusitisha mapigano.

Ikiwa siku moja baada ya mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa China kufanya ziara mjini Moscow na kuahidi ushirikiano wa dhati na Russia, Beijing ilijizuia kuonyesha msimamo wake katika kura hiyo, ikiwa ni mara ya nne kuchukua hatua kama hiyo tangu Russia iivamie Ukraine Februari 24 mwaka jana.

Azimio hilo lilipitishwa Alhamisi kwa kura 141 za kuliunga mkono na 32 za wanachama ambao hawakuonyesha msimamo wao.

Nchi sita ziliungana na Russia kwa kupinga azimio hilo. Nazo ni Belarus, Korea Kaskazini, Eritrea, Mali, Nicaragua na Syria.

“Azimio hili ni ishara kubwa ya kuungwa mkono kimataifa kwa Ukraine,” Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy aliandika ujumbe huo kwenye Twitter baada ya kura hiyo.

XS
SM
MD
LG