Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Februari 10, 2025 Local time: 04:42

Ulimwengu waadhimisha Siku ya Kimataifa ya Afya ya Akili


Mfanyakazi wa afya akitoa huduma kwa mgonjwa wa akili kwenye eneo la Srinagar, Kashmir linalodhibitiwa na India. Aug 1, 2023.
Mfanyakazi wa afya akitoa huduma kwa mgonjwa wa akili kwenye eneo la Srinagar, Kashmir linalodhibitiwa na India. Aug 1, 2023.

Jumatatu ulimwengu umesdhimisha siku ya kimataifa ya Afya ya Akili kauli mbiu ikiwa ni “Afya ya Akili ni haki ya msingi ya kila binadamu.” Shirika la Afya duniani WHO limesema kwamba watu wenye matatizo ya afya ya akili kote ulimwenguni wanapitia hali fulani ya ubaguzi. 

Kupitia taarifa iliyotolewa, WHO imesema kwamba kuwepo na changamoto za afya ya akili hakuwezi kuchukuliwa kama sababu ya kumnyima mtu haki yake ya kibinadamu, au kumuengua kwenye maamuzi muhimu kuhusiana na afya yake. Licha ya hilo, watu wenye matatizo ya kiakili kote ulimwenguni wameendelea kushuhudia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, taarifa imeongeza.

WHO imesema kwamba mtu mmoja kati ya kila 8 ulimwenguni anaishi na tatizo la afya ya akili, ambayo huenda ikaathiri afya ya mwili, hali yao ilivyo, pamoja na kuathiri maisha yao kwa ujumla. Siku ya kimataifa ya afya ya akili ilianzishwa 1992 na shirikisho la kimataifa la Afya ya Akili, na tangu wakati huo imeendelea kupata umaarufu, wakati watu zaidi wakiendelea kuhamasika kuhusu umuhimu wa afya ya akili katika uzima wa mwili wa binadamu.

Shirika hilo limekuwa likihamasisha kuhusu mahitaji ya watu wanaopitia changamoto za afya ya akili tangu 1948.

Forum

XS
SM
MD
LG