Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 02:55

Uingereza yasema kundi la kwanza la wahamiaji watafahamishwa nia ya serikali kuwahamishia Rwanda


Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson.
Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson.

Uingereza imesema kwamba kundi la kwanza la wahamiaji wasio na haki ya kuishi nchini  Uingereza wiki hii watafahamishwa kuhusu nia ya serikali kuwahamishia Rwanda chini ya mpango mpya wa uhamiaji.

Serikali ya Uingereza ambayo mwezi uliopita ilipanga kuwapeleka wanaotafuta hifadhi katika taifa hilo la Afrika mashariki la Rwanda, imesema kwamba ilitarajia wanasheria wanao kuwakilisha baadhi yao kuwasilisha madai yatakayo wazuia kuondolewa nchini humo, ambapo ndege ya kwanza inatarajiwa kuondoka katika kipindi cha miezi michache ijayo.

Hii ni hatua ya kwanza ya mchakato, na tunafahamu itachukuwa muda kutokana na kwamba baadhi yao watataka kuuvuruga mpango huo na kuchelewesha watu hao kupelekwa Rwanda, alisema waziri wa mambo ya ndani, Priti Patel katika taarifa.

XS
SM
MD
LG