Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Machi 26, 2025 Local time: 22:04

Uingereza kuanza tena program ya chanjo za Covid-19, baada ya kugundulika kwa aina mpya ya kirusi.


Picha ya chupa zenye chanjo ya Covid-19
Picha ya chupa zenye chanjo ya Covid-19

Uingereza itaanza program ya utoaji chanjo za mafua na Covid-19 wakati wa mwanzo wa msimu wa baridi kama tahadhari baada ya kugundulika kwa aina mpya ya kirusi cha Covid cha BA.2.86.

Wanasayansi wanasema kwamba kirusi cha BA.2.86, ambacho ni kutokana na kile cha Omicron huenda kisisababishe maradhi au vifo kutokana na kinga iliyoletwa na chanjo za awali kote ulimwenguni. Hata hivyo wizara ya afya ya Uingereza imesema kwamba program ya chanjo ya kila mwaka kwa wakongwe pamoja na makundi yaliopo hatarini itaanza wiki kadhaa kabla ya muda wake kutokana na kirusi hicho kipya.

Kirusi hicho kiligundulika mara ya kwanza Uingereza hapo Agosti 18, wakati zoezi la chanjo likipangwa kuanza Septemba 11, miongoni mwa wakazi waliyopo kwenye nyumba za wazee, pamoja wa wale waliyopo kwenye hatari zaidi ya maambukizi. Wizara hiyo imeongeza kusema kwamba bado kirusi hicho hakijaorodheshwa kuwa hatari nchini humo, na kwa hivyo hakuna haja ya kuweka kanuni mpya za kuzuia maambukizi kwa umma.

Forum

XS
SM
MD
LG