Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 13:46

Uhispania, Ureno na Iran zasubiri


Mshabiki wa soka katika uwanja wa Luzhniki, uliopo Moscow Russia, wakati wa mchezo wa Ureno na Morocco, Jumatano, Juni 20, 2018.
Mshabiki wa soka katika uwanja wa Luzhniki, uliopo Moscow Russia, wakati wa mchezo wa Ureno na Morocco, Jumatano, Juni 20, 2018.

Timu za Ureno, Uhispania, na Iran zitasubiri michezo yake ya mwisho kujua hatma zao za kusonga raundi ya pili huku Morocco ikiaga michuano ya Kombe la Dunia Russia 2018.

Kutokana na idadi ya pointi katika kundi B, timu yoyote inaweza kuifuata Morocco kurejea nyumbani. Uhispania inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 4, Ureno pointi 4 na Iran ikiwa na pointi 3.

Japokuwa timu ya Iran ilipoteza mchezo wake wa pili dhidi ya Uhispania Jumatano, ushindi dhidi ya Ureno katika mchezo wake wa mwisho unaweza kuifanya timu hiyo kuwa na pointi 6 na kufuzu.

Heka heka langoni mwa Iran, wakati wa mchezo wake dhidi ya Uhispania. Iran ilipoteza mchezo kwa kufungwa (1 - 0) na Uhispania, Jumatano, Juni 20, 2018.
Heka heka langoni mwa Iran, wakati wa mchezo wake dhidi ya Uhispania. Iran ilipoteza mchezo kwa kufungwa (1 - 0) na Uhispania, Jumatano, Juni 20, 2018.

Mpaka sasa timu zilizo ingia raundi ya pili ni wenyeji Russia na Uruguay kuktoka kundi A, huku Saudi Arabia na Misri zikishindwa kuvuka raundi ya pili ya mtoano.

Magoli ya Christiano Ronaldo kwa Ureno, na Diego Costa kwa Uhispania yalizipa nafasi nzuri timu hizo ya kusonga mbele baada ya mchezo wa kwanza kutoka suluhu (3-3).

Mfungaji wa goli la Ureno Christiano Ronaldo akifanya mashambulizi langoni mwa Morocco, Jumatano, Juni 20, 2018. Ronaldo mpaka sasa amefunga magoli manne katika michuano hii ya Kombe la Dunia 2018.
Mfungaji wa goli la Ureno Christiano Ronaldo akifanya mashambulizi langoni mwa Morocco, Jumatano, Juni 20, 2018. Ronaldo mpaka sasa amefunga magoli manne katika michuano hii ya Kombe la Dunia 2018.

Alhamisi itashuhudia michezo ya kundi C na D ambapo mpaka mwisho wa siku mwelekeo wa kundi C utafahamika. Denmark itacheza na Australia, Ufaransa na Peru na Argentina itapambana na Croatia.

XS
SM
MD
LG