Maambukizi ya Ebola yamesambaa na kuripotiwa katika jiji la Kampala.
Kaimu mkurugenzi wa kituo hicho Ahmed Ogwell Ouma, amesema kwamba maambukizi ya ebola nchini Uganda yamedhibitiwa.
Ouma pia amesema kwa sasa ni vigumu kutabiri mwenendo wa maambukizi ya virusi hivyo.
Maambukizi ya Ebola aina ya Sudan, visivyokuwa na chanjo yamekuwa yakisambaa nchini Uganda, tangu mwezi Septemba.
Watu 30 wamefariki kutokana na Ebola kote Uganda, huku maambukizi yakiongezeka na kufikia 109, wakiwemo watoto sita kutoka familia moja ambao wamegunduliwa kuambukizwa leo Alhamisi, katika jiji la Kampala.