Jumla ya walalamikajii 13, kikiwemo kituo cha televisheni cha mtandaoni, waliwasilisha shauri hilo katika mahakama ya katiba juu ya sheria hiyo, ambayo ilitiwa saini na kuwa sheria na Rais Yoweri Museveni wiki iliyopita.
Sheria hiyo ya kutumia vibaya intaneti “inatishia uhuru wa kujieleza na inalenga wale ambao wana maoni tofauti na serikali”, moja wa walalamikaji, Norman Tumuhimbise ameliambia shirika la habari la AFP.
Kulingana na ombi hilo, serikali imepewa siku saba kuwasilisha utetezi wake lakini haijulikani lini kesi hiyo itaanza kusikilizwa