Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 20:04

Uganda kutangaza awamu ya tatu ya utoaji leseni ya mafuta


Rais wa Uganda Yoweri Museveni akihudhuria mkutano na waandishi wa habari kufuatia mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov huko Entebbe, Uganda Julai 26, 2022
Rais wa Uganda Yoweri Museveni akihudhuria mkutano na waandishi wa habari kufuatia mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov huko Entebbe, Uganda Julai 26, 2022

Uganda ilisema siku ya Ijumaa inapanga kutangaza awamu ya tatu ya utoaji leseni ya mafuta mwezi Mei katika juhudi za kuendeleza zaidi sekta ya kuzalisha mafuta yake ya kwanza mwaka 2025.

Waziri wa Nishati Ruth Nankabirwa Ssentamu alisema katika taarifa yake akifafanua maendeleo katika sekta hiyo kwamba duru ijayo ya utoaji leseni itatangazwa katika mkutano wa kikanda wa mafuta ya petroli utakaofanyika katika mji mkuu wa Uganda Kampala mwezi Mei.

Hakusema ni vitalu vingapi vitapigwa mnada.

Nchi hiyo ya Afrika Mashariki iligundua akiba ya hidrokabon za kibiashara karibu na mpaka wake wa magharibi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwaka 2006. Uzalishaji unatarajiwa kuanza mwaka 2025.

Uganda pia inajenga bomba la kusafirisha mafuta ghafi na kiwanda cha kusafisha mafuta ghafi cha ndani ambacho kitasaidia kufanya rasilimali za mafuta nchini humo kuwa za kibiashara.

XS
SM
MD
LG