Ripoti zinaendelea kusema kwamba viwango huenda vikaongezeka mara nne kufikia 2040, iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa. Kulingana na ripoti hiyo, takriban chembechembe trilioni 171 za plastiki zilikuwa baharini kufikia 2019.
Utafiti huo ulikusanya data za uchafu wa plastiki kwenye maji ya bahari kutoka vituo 11,777, na kwenye maeneo 6 muhimu ya bahari kuanzia 1979 hadi 2019. Marcus Eriksen ambaye ni mwanzilishi mwenza wa 5 Gyres amesema kwamba kunahitajika mkataba wenye nguvu kutoka kwa Umoja wa Mataifa unaositisha uchafuzi wa plastiki kote ulimwenguni kwa kudhibiti vyanzo vyake.
Wataalam wamesema kwamba ripoti hiyo imefichua kwamba tatizo la uchafuzi wa plastiki kwenye bahari halijapewa uzito unaohitajika.
Facebook Forum