Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:35

Ubalozi wa Marekani wafuatilia hukumu ya kifo inayowakabili raia watatu


Adam Boehler.
Adam Boehler.

Marekani inasema ubalozi wake wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, unaendelea kufuatilia kwa karibu  kesi ya kisheria inayowahusu raia watatu wa Marekani ambao wanakabiliwa na hukumu ya kifo.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilikataa kutoa maoni yake kama kuna mazungumzo yanayo endelea ili kuachiliwa kwa Wamarekani hao.

Mwishoni mwa wiki, mjumbe maalum wa Rais wa Marekani, anaye shughulikia mateka, Adam Boehler, aliandika katika mtandao wa kijamii kwamba Wamarekani hao watatu bado wanashikiliwa na serikali ya DRC.

Raia wa Marekani wanaoshikiliwa DRC kutoka kushoto Tyler Thompson Jr., Marcel Malanga na Benjamin Reuben Zalman-Polun, kulia,
Raia wa Marekani wanaoshikiliwa DRC kutoka kushoto Tyler Thompson Jr., Marcel Malanga na Benjamin Reuben Zalman-Polun, kulia,

Septemba 2024, mahakama ya kijeshi nchini DRC iliwahukumu kifo watu 37, wakiwemo Wamarekani watatu Tyler Thompson Jr., Marcel Malanga na Benjamin Reuben Zalman Polun kwa jaribio la mapinduzi yaliyoshindikana hapo Mei 2024.


Forum

XS
SM
MD
LG