Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:09

Trump amekubali uteuzi wa chama chake kuwania muhula wa pili madarakani


Rais Trump akikubali uteuzi wa chama chake kuwania muhula mwingine madarakani, Agosti 27,2020
Rais Trump akikubali uteuzi wa chama chake kuwania muhula mwingine madarakani, Agosti 27,2020

Rais Trump alitoa hotuba yake ya kukubali uteuzi katika bustani ya ikulu ya Marekani, White House mbele ya maelfu ya wajumbe na wafuasi wa chama cha Republikan, hotuba ambayo imerushwa moja kwa moja na televisheni.

Rais Donald Trump amekubali rasmi uteuzi wa chama chake cha Republican kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi utakaofanyika Novemba 3 mwaka huu akiwania awamu ya pili.

Rais Trump alitoa hotuba yake ya kukubali uteuzi katika bustani ya ikulu ya Marekani, White House mbele ya maelfu ya wajumbe na wafuasi wa chama cha Republikan, hotuba ambayo imerushwa moja kwa moja na televisheni.

Hatua hiyo inakuwa sasa rasmi mchakato wa uchaguzi na pilika-pilika zake kuanza kwa kufanyika kampeni za kuomba kuchaguliwa kuongeza muhula mwingine, akipambana na mpinzani wake Joe Biden wa chama cha Democratic.

XS
SM
MD
LG