Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 13:25

Thailand yajadiliana na maafisa wa serikali mbalimbali kuhusu raia zao


(FILES) "Waathirika" wa vituo vya utapeli huko Kyauk Khet nchini Myanmar wakiwa katika mstari wakienda kukutana na jeshi la Thai, Februari 12, 2025.
(FILES) "Waathirika" wa vituo vya utapeli huko Kyauk Khet nchini Myanmar wakiwa katika mstari wakienda kukutana na jeshi la Thai, Februari 12, 2025.

Serikali ya Thailand imesema Alhamisi kwamba inafanya majadiliano na maafisa wa serikali mbali mbali au maafisa wa balozi  za nchi ambazo raia wao wamekwama kwenye mpaka kati ya Thailand na Myanmar.

Wafanayakazi hao waliokolewa kutoka vituo vilivyokua vinafanya utapeli wa mitandao huko Myanmar.

Kituo cha Utapeli ambako raia wa China, Vietnam, Ethiopia wanaosadikiwa kuwa wamesafirishwa kupitia biashara haramu ya binadam Myanmar.
Kituo cha Utapeli ambako raia wa China, Vietnam, Ethiopia wanaosadikiwa kuwa wamesafirishwa kupitia biashara haramu ya binadam Myanmar.

Kundi la wanamgambo wa kibudha DKBA linasema liko tayari kuwakabidhi kwa jeshi la Mnyanmar zaidi ya watu 400 wanaodaiwa ni wafanyakazi wa vituo hivyo wengi wao kutoka nchi za Afrika, ili kurudishwa makwao.

Mkuu wa utawala wa DKBA amewaambia waandishi habari kwamba tatizo kubwa ni kwamba jeshi haliko tayari kuwapokea na kuwasafirisha nyumbani.

Wafanyakazi hao wanaosema walirubuniwa kwenda kufanya kazi katika vituo hivyo vya utapeli kwenye wilaya ya Myanmar inayopakana na Thailand ni raia wa karibu mataifa 22 na wengi wao ni kutoka Ethiopia.

Forum

XS
SM
MD
LG