Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Desemba 20, 2025 Local time: 15:28

Talibani imepiga marufuku kilimo cha Afyuni huko Afghanistan; UNODC inasema


Kilimo cha Afyuni nchini Afghanistan ambae ni mzalishaji mkubwa zaidi wa Heroin duniani
Kilimo cha Afyuni nchini Afghanistan ambae ni mzalishaji mkubwa zaidi wa Heroin duniani

Ofisi ya Umoja wa mataifa ya Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inakadiria wakulima wa Afghanistan wamepoteza zaidi ya dola bilioni 1 za mapato kutokana na mauzo ya Afyuni kutokana na kushuka kwa kasi, hali ambayo inaweza kusababisha athari mbaya za kiuchumi na kibinadamu kwa nchi maskini.

Umoja wa Mataifa umesema Jumapili kuwa Taliban kupiga marufuku dawa za kulevya nchini Afghanistan kumesababisha kushuka kwa asilimia 95 ya kilimo cha Afyuni nchini humo, ambapo hutumiwa kutengeneza Morphine na Heroin.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa za Kulevya na Uhalifu ilirekodi mkataba unaokaribiana na hali jumla ya uchumi wa Afyuni kwa Afghanistan katika utafiti wake wa hivi karibuni wa kilimo cha Afyuni.

UNODC inakadiria wakulima wa Afghanistan wamepoteza zaidi ya dola bilioni 1 za mapato kutokana na mauzo ya Afyuni kutokana na kushuka kwa kasi, hali ambayo inaweza kusababisha athari mbaya za kiuchumi na kibinadamu kwa nchi maskini.

Serikali ya Taliban ilipiga marufuku kilimo cha Afyuni nchini Afghanistan, ambayo ni mzalishaji mkubwa zaidi wa Heroin duniani, hapo mwezi Aprili mwaka jana.

Forum

XS
SM
MD
LG