Kwenye mahojiano na VOA mapema wiki hii, Rina Amiri alisema kwamba jumuia ya kimataifa imeweka bayana kwa utawala wa Taliban kwamba iwapo hautarejesha haki za wanawake na wasichana, hakutakuwa na maendeleo yoyote katika kurejesha uhusiano wa kawaida unaozingatiwa na utawala huo.
Amiri ambaye ni mwanadiplomasia mwenye uzoefu mwingi, na ambaye amewahi kushikilia nyadhifa kadhaa kwenye Umoja wa Mataifa, pia aliwahi kuwa mshauri mkuu wa mwakilishi maalum wa Marekani nchini Afghanistan na Pakistan, Richard Holbrooke, wakati wa utawala wa Obama.
Maelfu ya wanawake walipoteza ajira zao baada ya Taliban kuchukua usukani mjini Kabul, wakati pia sera kandamizi dhidi ya wanawake zikibuniwa.
Facebook Forum