Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Machi 26, 2025 Local time: 22:05

Taiwan kuimarisha uhusiano wake na mataifa ya Baltic


Waziri wa mambo ya kieni wa Taiwan, Joseph Wu
Waziri wa mambo ya kieni wa Taiwan, Joseph Wu

Waziri wa mambo ya kigeni wa Taiwan Joseph Wu, anafanya ziara ya kidiplomasia kwenye mataifa ya Baltic wiki hii, wakati akitoa hotuba kwa makundi ya utafiti huko Latvia na Estonia, huku pia akibadilishana maoni kuhusu njia ya kuimarisha ushirikiano kati ya wabunge wa mataifa yote matatu.

Baadhi ya wachambuzi wanasema kwamba ziara hiyo ni moja wapo ya njia za kuimarisha uhusiano uliyojengwa na Taiwan kwa mataifa ya Baltic, tangu kufungiliwa kwa ofisi ya uwakilishi huko Lithuania, miaka miwili iliyopita.

Ziara hiyo imekuja baada ya Estonia kutangaza wiki iliyopita kwamba ingeruhusu Taiwan ifungue ofisi isiyo ya kidiplomasia kwenye mji mkuu wa Tallinn, kwa lengo la kuimarisha uhusinao wa kibiashara na utamaduni kati ya mataifa yote mawili.

Kupitia taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya kigeni Novemba 3, waziri wake Margus Tsahkna alifichua kuwa baraza la mawaziri lilitadhmini namna ya kuhusiana na Taiwan kwenye kikao.

Forum

XS
SM
MD
LG