Chama cha All People’s Congress ( APC) kimemchagua Kamara, ambaye alishindwa na Rais Julius Maada Bio katika uchaguzi uliopita, kama mgombea kwenye kinyang’anyiro cha urais mwezi Juni.
Kuteuliwa kwa Kamara kunajiri licha ya tangazo la Mahakama kuu kwamba uamuzi utatolewa Alhamisi juu ya kesi ya ufisadi dhidi yake na watu wengine watano.
Mwezi Disemba mwaka wa 2021, Kamara alishtakiwa kwa matumizi mabaya ya zaidi ya dola milioni 2.5 pesa za umma katika kesi iliyohusishwa na ukarabati wa ubalozi mdogo wa New York alipokuwa waziri wa mambo ya nje.
Facebook Forum