Mamia ya watu wanaaminika kuwa ndani ya hoteli hiyo ya Grand Diamond City, kwenye mji wa Poipet karibu na mpaka wa Thailand, pale moto ulipozuka usiku wa kuamkia Alhamisi.
Picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha watu wakiwa kwenye madirisha pamoja na paa la jengo hilo wakijaribu kuokoa maisha yao. Afisaa mmoja wa polisi wa Cambodia ameambia shirika la habari la AFP kwamba inaaminika kuwa watu wengi wamekwama ndani ya jengo hilo, huku waokozi wakiendelea kuwasaka.
Mamia ya wanajeshi , polisi pamoja na watu wa kujitolea wapo kwenye eneo la tukio wakiendelea na shuguli za uokozi. Ripoti zimeongeza kusema kwamba moshi uliendelea kutoka kwenye jengo hilo mapema Ijumaa, huku magari ya kuzima moto yakibaki chonjo. Wengi wa waliojeruhiwa wamepelekwa Thailand kwa matibabu wakati 13 miongoni mwao wakisemekana kuwa kwenye hali mahututi.