Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 14:11

Shirika la ICRC kusitisha ufadhili wake kwenye hospitali 25 nchini Afghanistan



Nembo ya Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu. ICRC.
Nembo ya Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu. ICRC.

Msemaji wa shirika la kimataifa la Msalaba Mwekundu, ICRC, amesema kwamba huenda wakasitisha msaada wa kifedha kwenye hospitali 25 nchini Afghanistan kufikia mwishoni mwa mwezi huu kutokana na uhaba wa ufadhili, huku kukiwa na wasiwasi wa kupungua kwa misaada kwa ujumla katika taifa hilo.

Msemaji wa ICRC Diogo Alcantara nchini Afghanistan amesema ingawa wanaendelea kushauriana na wizara za serikali, wafadhili pamoja na mashirika ya kimataifa kubuni mikakati mbadala ya kuendesha sekta ya afya, program hiyo maalum ya Hospitali inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi Agosti.

Amesema kwamba ICRC haina mamlaka wala rasilimali za kuendesha mfumo mzima wa afya kwa muda mrefu nchini humo.

Mwezi Aprili bodi ya ICRC iliidhinisha msaada wa dola milioni 475.30 zikilenga kupunguza gharama ya huduma za kimatibabu mwaka huu na mwaka ujao, pamoja na kupunguza operesheni katika baadhi ya vituo kutokana na matarajio kwamba bajeti za misaada ya kibinadamu zingepungua.

Kumalizika kwa progam hiyo kunatokea wakati kuna wasi wasi kutokana na kupunguzwa kwa misaada mingine ya kibinadamu nchini Afghanistan, miaka miwili baada ya Taliban kuchukua madaraka.

Misaada mingine ya kimataifa ambayo ilikuwa imeshikilia uchumi wa taifa hilo ilisitishwa kuanzia wakati huo.

Forum

XS
SM
MD
LG