Maafisa kwenye jimbo la mbali la kusini mwa Afghanistan la Helmand wanasema kundi la wapiganaji wa Taliban wasiopungua 10 wenye silaha nzito wamefanya mashambulizi yaliyopangwa kufanyika kwa wakati mmoja na kuzusha mapambano ya bunduki na vikosi vya usalama.
Shambulizi la mapema Jumanne katika wilaya ya Girishk lililenga makao makuu ya polisi na ofisi za Idara ya Upelelezi huko Afghanistan.
Mashambulio hayo yamesababisha kifo cha polisi mmoja na wengine kujeruhiwa.