Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 19:12

Watu 150 wafariki katika shambulizi la anga Somalia


FILE - Al-Shabab fighters are seen marching with their weapons during exercises on the outskirts of Mogadishu, Somalia, Feb. 17, 2011. The Pentagon says a U.S. airstrike against al-Shabab in Somalia last Saturday killed more than 150 militants.
FILE - Al-Shabab fighters are seen marching with their weapons during exercises on the outskirts of Mogadishu, Somalia, Feb. 17, 2011. The Pentagon says a U.S. airstrike against al-Shabab in Somalia last Saturday killed more than 150 militants.

Msemaji wa White house, Josh Earnest, alithibitisha jana kwamba kulikuwa na shambulizi la anga huko kaskazini ya Mogadishu.

Msemaji wa kundi la Al-Shabaab Somalia Sheikh Abdiasis Abu Musab anaripotiwa kukiri kutokea shambulizi la anga la Marekani katika kambi yake iitwayo Raso kaskazini mwa Mogadishu .

Lakini aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba idadi ya majeruhi iliyotolewa jumatatu ya kuuliwa watu 150 kutokana na shambulizi hilo la Jumamosi ni uwongo kwani anasema ni idadi kubwa kuliko waliofariki.

Msemaji wa White house, Josh Earnest, alithibitisha jana kwamba kulikuwa na shambulizi la anga huko kaskazini ya Mogadishu.

Pentagon imeeleza kwamba ndege zote zisizo na rubani na zilizo na rubani zilitumika kwenye shambulizi hilo kwenye kambi kaskazini mwa mji mkuu wa Somalia. Ilieleza katika taarifa yake kwamba walitumia taarifa za kijasusi na walikuwa wakifuatilia shughuli katika kambi hiyo kwa wiki kadhaa.

XS
SM
MD
LG