Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 15:11

Shambulio la anga lapiga karibu na hospitali katika mji wa Mekelle


Wanajeshi wa serikali ya Ethiopia wakipanda nyuma ya lori kwenye barabara karibu na Agula, kaskazini mwa Mekele, katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia Mei 8, 2021. (AP Photo/Ben Curtis).
Wanajeshi wa serikali ya Ethiopia wakipanda nyuma ya lori kwenye barabara karibu na Agula, kaskazini mwa Mekele, katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia Mei 8, 2021. (AP Photo/Ben Curtis).

Shambulio la anga limepiga karibu na hospitali moja katika mji mkuu wa mkoa wa Tigray kaskazini mwa Ethiopia, alisema mkuu wa hospitali nyingine ambayo ilipokea majeruhi, chini ya wiki moja baada ya mapigano kusambaratisha usitishaji mapigano wa miezi minne.

Wakiwa katika vita tangu mwishoni mwa mwaka 2020, chama cha Tigray People's Liberation Front (TPLF), ambacho kinadhibiti eneo hilo, na serikali kuu ya Waziri Mkuu Abiy Ahmed wamelaumiana kwa mzozo mpya ambao unazuia msaada wa chakula unaohitajika sana.

Kibrom Gebreselassie, mtendaji mkuu wa Hospitali Kuu ya Ayder, alitweet kwamba eneo karibu na Hospitali Kuu ya Mekelle lilishambuliwa Jumanne jioni.

Kiwango cha uharibifu na majeruhi hakikuwa wazi.

Msemaji wa serikali ya Ethiopia Legesse Tulu, msemaji wa jeshi Kanali Getnet Adane na msemaji wa waziri mkuu Billene Seyoum hawakujibu maombi ya maoni yao.

Getachew Reda, msemaji wa TPLF, alisema kwenye Twitter kwamba takriban mabomu matatu yamerushwa na kwamba hospitali ya Mekelle ni miongoni mwa walengwa.

XS
SM
MD
LG