Serikali ya Uganda imekiri kukumbwa na changamoto ya kudhibiti uchumi wan chi yake. Hayo yamesemwa na waziri wa fedha wa Uganda kwamba hali ya uchumi ni ngumu kwa wakati huu nchini humo.
Kampuni kadhaa zimekimbilia serikalini zikitaka msaada wa fedha ambapo wafanyakazi katika baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali-NGOs walikosa mishahara kwa zaidi ya takribani miezi miwili.
Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika-VOA mjini Kampala huko Uganda alifuatilia taarifa hii na kututumia ripoti zaidi ya kile kinachojiri kwenye suala la uchumi nchini humo.