Serikali ya Uganda imesema kwamba haiwezi kuruhusu ukaguzi wa kina wa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Februari kama anavyotaka mpinzani wa kisiasa Dr. Kiiza Besigye na chama chake cha Forum for Democratic Change-FDC.
Kulingana na serikali ni kwamba ukaguzi huo unatofautiana na sheria, kwani maamuzi ya mwisho kuhusu uchaguzi yalitolewa na mahakama kuu nchini humo.
Serikali pia ilisema sasa ipo tayari kukabiliana na kiongozi huyo wa upinzani Dr. Besigye kama mtu binafsi iwapo ataendelea na harakati zake za kupinga matokeo ya uchaguzi huo.
Mwandishi wa VOA kutoka kampala, Kennes Bwire anaripoti zaidi.