Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 12:42

Serikali ya Ethiopia yaahidi kushiriki mazungumzo ya amani na waasi wa Tigray, lakini yakaa kimya kuhusu kusitisha mapigano


Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed
Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed

Serikali ya Ethiopia Jumatatu imeelezea tena dhamira yake ya kushiriki kwenye mazungumzo ya amani kuhusu mzozo wa Tigray, lakini haikujibu wito wa Umoja wa Afrika wa kusitisha mapigano, ikiahidi badala yake kuchukua hatua za kujihami.

Jumapili, mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahmat alitoa wito wa sitisho la mapigano mara moja na bila masharti yoyote, wakati mapigano yakiongezeka katika mkoa wa Tigray, na kuzitaka pande hizo mbili ambazo zinapigana kwa karibu miaka miwili kukubali tena kufanya mazungumzo.

Viongozi wa Tigray Jumapili wamesema wako tayari kutekeleza sitisho la mara moja la uhasama na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuishinikiza serikali ya Ethiopia kufika kwenye meza ya mazungumzo.

Addis Ababa Jumatatu imesema ina dhamira ya kutatua mzozo huo kwa njia ya amani kupitia mazungumzo yanayoongozwa na Umoja wa Afrika.

XS
SM
MD
LG