Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 09:32

Serikali ya Congo yawalaumu waasi wa M23 kwa shambulizi dhidi ya helikopta


Waasi wa kundi la M23 wakifanya mazoezi huko Rumangabo, Mashariki mwa Congo.Katika picha hii iliyopigwa Jumanne, Oktoba 23, 2012.
Waasi wa kundi la M23 wakifanya mazoezi huko Rumangabo, Mashariki mwa Congo.Katika picha hii iliyopigwa Jumanne, Oktoba 23, 2012.

Serikali ya Congo siku ya Jumatatu iliwalaumu waasi wa M23 kwa shambulizi dhidi ya helikopta na kumuua mwanajeshi wa  kulinda amani wa Umoja wa Mataifa, huku mamia ya watu katika mji wa mashariki wa Goma wakiandamana kutokana na kukithiri kwa ukosefu wa usalama katika eneo hilo.

Ghasia za wanamgambo zimekumba eneo kubwa la mashariki lenye utajiri mkubwa wa madini la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa miongo miwili licha ya uingiliaji kati wa kijeshi wa ndani na kikanda na juhudi za kulinda amani za Umoja wa Mataifa.

Helikopta iliyokuwa ikiendeshwa na kikosi cha kulinda amani cha MONUSCO ilishambuliwa siku ya Jumapili baada ya kuruka kutoka mji wa Beni. Mlinda amani wa Afrika Kusini aliuwawa na mwingine mmoja kujeruhiwa.

Si Afrika Kusini wala MONUSCO iliyosema ni nani anaweza kuwa anahusika, wala ni aina gani ya silaha iliyotumika kuilenga helikopta hiyo au ni nini kilisababisha majeruhi.

Serikali ya Kinshasa ilililaumu kundi la M23 katika taarifa yake siku ya Jumatatu. Kundi hilo ambalo lilianzisha mashambulizi makubwa mwaka jana, lilikanusha sgutuma hizo.

Ikiwa na takriban wafanyakazi 18,200, MONUSCO imetumwa mashariki mwa Congo tangu kuchukua nafasi ya operesheni ya awali ya Umoja wa Mataifa mwaka 2010. Jukumu lake ni pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali ya Congo kuleta utulivu katika eneo hilo.

XS
SM
MD
LG