Kampuni kubwa ya vifaa vya elektronki ya Samsung iliyoi na makao yake makuu Korea Kusini, ilisema siku ya Jumanne kuwa haitatengeneza tena simu aina ya Galaxy Note 7 kutokana na matatizo yaliyojitokeza kufuatia ripoti kadhaa kote ulimwenguni kuhusu kupata joto sana kwa simu hiyo. L
Kampuni hiyo ilitangaza kufunga kabisa utengenezaji kwa maslahi ya usalama wa mnunuzi. Samsung awali ilitangaza kwamba inasitisha mauzo yote ya galaxt note 7 kote ulimwenguni na kuwashauri wateja wake kuacha haraka kutumia kifaa hicho.
Samsung imepata hasara ya asilimia 8 katika hisa zake katika soko la hisa wakati wa kufunguliwa kwa biashara hivi leo. Makampuni kadhaa makubwa ya simu za mkononi ikiwemo kampuni ya AT & T yenye makao yake hapa marekani na ya ujerumaini ya T-Mobile kila moja imetangaza jumapili kuwa imesitisha mauzo au kubadilisha simu ya galaxy note 7.