Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 14:08

Safaricom ya Kenya yazindua mtandao wake wa simu nchini Ethiopia


Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed, na rais wa Kenya William Ruto wakihudhuria uzinduzi rasmi shughuli za kampuni hiyo mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed, na rais wa Kenya William Ruto wakihudhuria uzinduzi rasmi shughuli za kampuni hiyo mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Safaricom ya Kenya, ilizindua mtandao wake wa simu nchini Ethiopia siku ya Alhamisi, na kuwa kampuni ya kwanza ya kibinafsi kufanya hivyo katika mojawapo ya soko kubwa zaidi la mawasiliano barani Afrika.

Ethio Telecom inayomilikiwa na serikali ya Ethiopia hadi sasa imefurahia kuwa peke yake nchini Ethiopia, nchi ya pili barani Afrika kwa kuwa na watu wengi zaidi, ikikadiriwa kuwa watu milioni 118.

Safaricom Ethiopia iliwasha mtandao na huduma zake katika mji mkuu Addis Ababa siku ya Alhamisi kufuatia huduma za majaribio za mtandao huo katika miji 10, ilisema katika taarifa.

Saa chache baadaye waziri wa fedha wa Ethiopia, Ahmed Shide, alisema serikali yake iliipa kampuni hiyo leseni ya kuendesha huduma ya pesa kwa njia ya simu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Safaricom Ethiopia Anwar Soussa alisema huduma hiyo ya pesa kwa njia ya simu itachukua miezi miwili hadi mitatu kutekelezwa.

Safaricom inaongoza muungano unaoingia sokoni ikiwa ni pamoja na Vodacom ya Afrika Kusini na Vodafone ya Uingereza.

Mtandao wake ulipaswa kuzinduliwa mwezi Aprili lakini ulicheleweshwa kwa sababu ya janga la corona na changamoto za vifaa.

XS
SM
MD
LG