Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 10:10

Russia imeunganisha rasmi maeneo inayoyakalia kimabavu ya Ukraine


Waokoaji wanatumia kreni kuondoa vifusi vya jengo la ghorofa lililoharibiwa na makombora ya Russia huko Donetsk, Ukraine inayodhibitiwa na Russia, Februari 4, 2023. REUTERS.
Waokoaji wanatumia kreni kuondoa vifusi vya jengo la ghorofa lililoharibiwa na makombora ya Russia huko Donetsk, Ukraine inayodhibitiwa na Russia, Februari 4, 2023. REUTERS.

Russia imeunganisha rasmi maeneo inayoyakalia kimabavu ya Ukraine katika Wilaya ya Kijeshi ya Kusini mwa nchi hiyo  Wizara ya Ulinzi ya Uingereza ilisema Jumamosi katika ripoti yake ya kila siku ya kijasusi.

Shirika hilo lilisema habari za kuunganishwa huko zinatokana na ripoti ya Tass kwamba mikoa ya Donetsk na Luhansk na mikoa ya Zaporizhzhia na Kherson imewekwa chini ya usimamizi wa kamandi ya kijeshi ya nyota tatu iliyoko Rostov-on-Do.

Ripoti hiyo ilisema, hata hivyo, hatua hiyo haina uwezekano wa kuwa na athari za haraka katika uvamizi wa Russia nchini Ukraine.

Kundi la Nchi Saba zilizoendelea kiviwanda duniani zilikubaliana Ijumaa juu ya kukomo wa bei ya usafirishaji wa mafuta yaliyosafishwa ya Russia.

Waziri wa Fedha wa Marekani Janet Yellen alisema katika taarifa yake kwamba makubaliano hayo yanafuata kikomo sawa cha bei kwa mauzo ya mafuta ghafi ya Russia kilichowekwa mwezi Desemba na kusaidia kuendeleza malengo yao ya kuzuia kitu kikuu kinachoingiza mapato ya Russia katika kufadhili vita vyake haramu nchini Ukraine.

XS
SM
MD
LG