Mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 37 alijiunga na klabu hiyo mwezi uliopita kwa mkataba utakaodumu hadi 2025, akiripotiwa kulipwa zaidi ya paundi milioni 177 kwa mwaka.
Aliongoza na kucheza mechi nzima ambapo kiungo wa Brazil Anderson Souza Conceição, au Talisca alifunga bao la ushindi.
Al Nassr wako kileleni mwa ligi ya Saudia Arabia wakiwa na pointi moja juu ya Al Hilal iliyo nafasi ya pili.
Ronaldo ambaye aliwahi kuzichezea Manchester United, Juventus na Real Madrid alilakiwa na mabango na shangwe kutoka kwa mashabiki wake na wapenzi kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha King Saud mjini Riyadh.