Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 15:34

RED-Tabara wadai kufanya mauaji ya watu 20 nchini Burundi


Baadhi ya wapiganaji wa kundi la uasi la RED-Tabara waliokamatwa. Picha ya maktaba
Baadhi ya wapiganaji wa kundi la uasi la RED-Tabara waliokamatwa. Picha ya maktaba

Serikali ya Burundi imesema Jumamosi  kwamba shambulizi la waasi magharibi mwa nchi limeua watu 20 wote wakiwa raia isipokuwa mmoja. Kundi la Red-Tabara limedai kuhusika wakati kupitia taarifa yake likisema kwamba limeuwa maafisa 10 wa usalama.

Shambulizi hilo la Ijumaa jioni limefanyika kwenye mji wa Vugizo karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrais ya Congo, ambao ni ngome ya kundi hilo. Serikali imeongeza kusema kwamba shambulizi hilo la 'kigaidi na la kikatili,' lililenga raia, wakati likiua watoto 12, wakiwemo watano waliyopo chini ya umri wa miaka 5, wanawake watatu wakiwawemo wawili wajawazito na wanaume watano akiwemo polisi mmoja aliyekuja kuwasidia.

Watu wengine 9 wajeruhiwa wakati wakiendelea kupokea matibabu hospitalini. Kundi la RED- Tabara kupitia ujumbe wa X iliyojulikana awali kama Twitter, limesema kwamba wapiganaji wake waliyopo Burundi wameshambulia kituo cha mpakani cha Vugizo, na kwamba wanajeshi 9 na polisi mmoja wameuliwa. Vyanzo viwili vya kijsehi na kiusalama vimeambia shirika la habari la AFP kwamba shambulizi hilo lililenga kituo cha kijeshi

Forum

XS
SM
MD
LG