Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 20, 2023 Local time: 19:24
VOA Direct Packages

Rais wa Peru awasilisha mswaada mpya utakaoruhusu kuitishwa uchaguzi kwa haraka


Rais wa Peru Dina Boluarte

Rais wa Peru Dina Boluarte amewasilisha mswaada mpya utakaoruhusu kuitishwa kwa uchaguzi mwaka huu kama hatua ya kuituliza nchi, baada ya bunge kushindwa kukubaliana, huku siasa kali zikiendelea kwa wiki kadhaa sasa.

Mswaada huo ambao shirika la habari la Reuters umeuona unapendekeza kufanyika kwa uchaguzi wa bunge na rais Oktoba mwaka huu,na kisha waliochaguliwa wachukue madaraka hapo Desemba, wakati wakihudumu kwa muhula wa miaka mitano hadi 2028.

Taifa hilo kwa kipindi cha wiki 8 limeshuhudia maandamano makali dhidi ya serikali yaliyopelekea vifo vya takriban watu 48, wakati wa mapambano kati yao na maafisa wa usalama, na hasa kwenye maeneo ya kusini yenye utajiri mkubwa wa madini ya shaba.

Waandamanaji wamekuwa wakidai uchaguzi wa haraka uitishwe baada ya rais wa mrengo wa kushoto Pedro Castillo kuondolewa madarakani Desemba mwaka uliopita. Waziri mkuu Aberto Otarola anatarajiwa kuwasilisha mswaada huo kwenye tume maalum ya bunge baadaye Ijumaa. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya mapendekezo kadhaa ya kuitisha uchaguzi kufeli mbele ya bunge.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG