Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan ametoa mwito wa kumaliza ghasia kaskazini mwa nchi hiyo ambako kuna waislamu wengi kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa rais.
Katika hotuba yake Jumatatu jioni bwana Jonathan alisihi kuwepo umoja wa kitaifa akisema kuwa hakuna ushawishi wa kisiasa wa mtu yoyote ulio na thamani kuliko damu ya raia wa Nigeria yoyote.
Shirika la msalaba mwekundu limesema watu wengi wamekufa na maelfu kukoseshwa makazi Jumatatu wakati ghasia zilipozuka upande wa kaskazini kupinga matokeo ya uchaguzi.
Wafuasi wa upinzani wanadai kuwa kura ziliibiwa na wamechoma moto nyumba, matairi pamoja na kurushia mawe polisi.
Bwana Jonathani amepata kura nyingi kati ya asilimia 57 zilizohesabiwa hivyo kuepuka uchaguzi wa marudio.
Hakuna chama chochote cha upinzani kilichotia saini katika matokeo ya mwisho .