Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 17:42

Obama ataelezea mkakati wa kupambana na ISIS Iraq


Rais wa Marekani Barack Obama
Rais wa Marekani Barack Obama

Rais wa marekani Barack Obama ataelezea mkakati wake wa kupambana na kundi lenye msimamo mkali la Islamic State huko Irak na Syria katika hotuba kwenye televisheni Jumatano usiku.

Msemaji wa ikulu ya marekani Josh Earnest amesema bwana Obama anaamini kuwa hiki ni kipaumbele kikubwa cha usalama wa nchi.

Amesema rais atazungumzia kuhusu kitisho kinachotolewa na wanamgambo wa Islamic State na mpango wake wa kulidhalilisha na kulivunja kundi la Islamic State.

Ernest hajafafanua kitu alichopanga bwana Obama kuzungumzia, lakini rais Obama tayari amefuta uwezekano wa kurejesha majeshi ya Marekani nchini Iraq.

XS
SM
MD
LG