Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 10:15

Rais wa China kufanya ziara Russia katika juhudi za kumaliza vita vya Ukraine


Rais wa China Xi Jinping, na rais wa Russia Vladimir Putin, wakati wa mkutano nchini Uzbekistan, Septemba 15, 2022
Rais wa China Xi Jinping, na rais wa Russia Vladimir Putin, wakati wa mkutano nchini Uzbekistan, Septemba 15, 2022

Rais wa China Xi Jinping atafanya ziara nchini Russia wiki ijayo kwa mazungumzo na Rais Vladimir Putin, nchi hizo mbili zimesema leo Ijumaa, huku Beijing ikipongeza mpango Xi wa kujaribu kumaliza vita vya Ukraine.

Safari ya Xi kuanzia tarehe 20 hadi 22 Machi inajiri baada ya China kuchapisha mwezi uliopita mpango wenye vipengele 12 wa ‘suluhisho la kisiasa kwa ajili ya mzozo wa Ukraine’ na baada ya mwanadiplomasia mkuu wa China kutoa wito wa mazungumzo jana Alhamisi katika mawasiliano ya simu na waziri wa mambo ya nje wa Ukraine.

Mpango huo unatoa wito wa kuwalinda raia na kwa Russia na Ukraine kuheshimu uhuru wa kila mmoja wao.

Hata hivyo, Marekani na NATO wamesema juhudi za Beijing kupatanisha katika mzozo wa Ukraine sio za kuaminika kwa sababu imejizuia kulaani uvamizi wa Russia dhidi ya Ukraine, ambao Moscow inauita ‘operesheni maalum ya kijeshi.’

XS
SM
MD
LG