Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 21:55

Rais Ruto awateua majaji sita walioibua utata


Rais William Ruto (Kulia) na Jaji Mkuu wa Kenya Martha Karambu Koome.
Rais William Ruto (Kulia) na Jaji Mkuu wa Kenya Martha Karambu Koome.

Rais wa Kenya William Ruto, saa chache tu baada ya kuapishwa kama kiongozi wa taifa hilo la Afrika Mashariki, aliwateua majaji sita wa mahakama ya rufaa, waliokuwa wamependekezwa na Tume ya Huduma za Mahakama miaka mitatu iliyopita, lakini rais aliyemtangulia Uhuru Kenyatatta akakataa kuwidhinisha.

Ruto alisema majaji hao sita wataapishwa leo Jumatano katika Ikulu mjini Nairobi.

Rais pia aliahidi kutenga Sh3 bilioni za ziada kwa bajeti yake ya kila mwaka kila mwaka.

Bila kutoa maelezo zaidi, Rais wa zamani Uhuru Kenyatta alipuuza uteuzi wa majaji hao, miaka mitatu iliyopita akidai kuwa "walikuwa na dosari" na kuwateua wenzao 34 mnamo mwezi Juni 2021.

Ruto aliapishwa kama rais wa tano wa Kenya, wiki moja baada ya Mahakama ya Juu kuidhinisha uchaguzi ambao ulikatiza matumaini ya familia mashuhuri za kisiasa nchini humo na kumpa mamlaka mtu ambaye alilelewa katika mazingira ya umaskini, na kuanza kazi yake kama muuza kuku kando ya barabara.

Ruto, ambaye alihudumu kama naibu wa rais wa Kenya kwa miaka 10, anachukua hatamu za uongozi wakati gharama ya maisha ikiwa juu, huku kukiwa na ukosefu mkubwa wa ajira na kuongezeka kwa deni la umma.

Baada ya kuapishwa, Ruto aliahidi mambo kadhaa ambayo alisema angeyapa kipaumbele.

XS
SM
MD
LG