Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 07:54

Rais Museveni amuondoa Muhoozi kuongoza majeshi ya nchi kavu na kumpandisha cheo


Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amepandishwa cheo kutoka Luteni jenerali hadi Jenerali kamili na atasalia kuwa mshauri mkuu wa rais kwa operesheni maalum.
Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amepandishwa cheo kutoka Luteni jenerali hadi Jenerali kamili na atasalia kuwa mshauri mkuu wa rais kwa operesheni maalum.

Rais Yoweri Museveni amemuondoa mwanawe, Muhoozi Kainerugaba, kama kamanda wa majeshi ya nchi kavu ya Uganda, jeshi lilisema Jumanne, baada ya Kainerugaba kutishia mara kwa mara kwenye ukurasa wake wa Twitter kuivamia nchi jirani ya Kenya.

Kainerugaba, anayejulikana sana kama mkuu wa jeshi na mrithi aliyechaguliwa na baba yake, baadaye alisema maoni hayo yalitolewa kwa mzaha.

Katika taarifa iliyotangaza kubadilishwa kwake kama kamanda wa vikosi vya nchi kavu, jeshi lilisema Kainerugaba amepandishwa cheo kutoka luteni jenerali hadi jenerali kamili na atasalia kuwa mshauri mkuu wa rais kwa operesheni maalum. Haikutoa sababu ya uamuzi huo.

Kainerugaba anazungumza waziwazi kwenye mitandao ya kijamii, mara kwa mara akitoa vijembe kwa viongozi wa upinzani na kujikita katika siasa, licha ya jukumu lake la kijeshi kumzuia kufanya hivyo.

Jumatatu na Jumanne alituma msururu wa jumbe za uchochezi kwenye Twitter, zikiwemo kupendekeza kuunganishwa kwa Kenya na Uganda, na kutoa ng'ombe kwa mahari ya kumuoa kiongozi anayetarajiwa huenda akachukua madaraka huko Italia.

"Haingetuchukua sisi, jeshi langu na mimi, wiki 2 kuchukua Nairobi," Kainerugaba aliandika, akimaanisha mji mkuu wa Kenya.

XS
SM
MD
LG