Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 17:33

Rais Erdogan wa Uturuki ameshinda uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili


Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameshinda uchaguzi wa urais kupitia chama chake cha People's Alliance. May 28, 2023.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameshinda uchaguzi wa urais kupitia chama chake cha People's Alliance. May 28, 2023.

Erdogan alishinda Jumapili katika mzunguko wa pili wa upigaji kura kwa asimilia 52 akifuatiwa na mpinzani mkuu Kemal Kilicdaroglu aliyepata asilimia 47.8 ya kura

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ana muhula mpya wa miaka mitano baada ya kushinda uchaguzi wa marudio ambao wanachama wa upinzani walitumai huenda utamuondoa madarakani kufuatia ghasia zinazohusu ongezeko la gharama ya maisha.

Erdogan alishinda Jumapili katika mzunguko wa pili wa upigaji kura kwa asimilia 52 akifuatiwa na mpinzani mkuu Kemal Kilicdaroglu aliyepata asilimia 47.8 ya kura. "Ninamshukuru kila mwanachama katika taifa letu kwa kuendelea kuniamini kuchukua majukumu ya kui ongoza nachi hii kwa mara nyingine katika kipindi cha muhula wa miaka mitano", Erdogan aliwaambia wafuasi wake.

"Napenda kuwashukuru raia wetu wote ambao walionyesha nia zao za dhati kwa mustakbali wa baadae ya taifa hili, kwa ajili yao na watoto wao, kwa kupiga kura kwenye uchaguzi huu".

Kilicdaroglu hakupinga matokeo lakini aliuita uchaguzi usio sahihi katika miaka ya karibuni.

Forum

XS
SM
MD
LG