Baraza la kitaifa la kufuatilia utangazaji habari ( CNC) lilifuta leseni ya BBC mwaka wa 2019, likishtumu radio hiyo kukiuka sheria ya vyombo vya habari na kutofuata maadili ya utangazaji habari.
“Tumefikia uamuzi wa kuifungua tena radio BBC kuanzia leo,” mwenyekiti wa CNC Vestine Nahimana amesema.
Idhaa hiyo ilikidhi masharti yaliyowekwa na serikali, ameongeza.
Sauti ya America pamoja na BBC zote zilisimamishwa mwezi Mei mwaka wa 2018.
Idhaa hizo mbili zilisimamishwa wiki mbili kabla ya kura ya maoni ya kufanyia marekebisho katiba, ili kumruhusu rais wa zamani Pierre Nkurunziza kuongoza hadi mwaka wa 2034.