Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 00:20
VOA Direct Packages

Putin asifu uhusiano dhabiti uliyopo kati ya Russia na China


Rais wa Russia Vladimir Putin, (Kulia) akiwa kwenye kikao na waziri wa ulinzi wa China, Li Shangfu, mjini Moscow, April 16, 2023. (Sputnik via Reuters)
Rais wa Russia Vladimir Putin, (Kulia) akiwa kwenye kikao na waziri wa ulinzi wa China, Li Shangfu, mjini Moscow, April 16, 2023. (Sputnik via Reuters)

Rais wa Russia Vladimir Putin Jumapili amesifu uhusiano wa karibu wa taifa lake na China, ikiwemo ushirikiano wa kijeshi, wakati akifanya kikao na waziri wa ulinzi wa China Li Shangfu mjini Moscow.

Katika matamshi yake ya ufunguzi, Putin aliesema, ”Kuimarika kwa ushirikiano kati ya mataifa yetu kunaendelea vyema kwenye nyanja zote, zikiwemo kiuchumi, kijamii, kitamaduni, kielimu na hata kijeshi ." Kremlim ilirusha video fupi iliyomuonyesha Putin akisalimiana na Li na kisha kuketi kwenye meza moja.

Waziri wa ulinzi wa Russia Sergei Shoigu pia alikuwepo kwenye kikao hicho. Wiki iliyopita Beijing ilitangaza kuhusu ziara ya Li nchini Russia akisema kwamba angekutana na maafisa wa ulinzi , bila kutaja kwamba angekutana na Putin. Rais wa China Xi Jinping mwezi uliopita pia alikutana na Putin mjini Moscow.

XS
SM
MD
LG