Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 08:00

Putin asema kwamba Russia haitaondoka Ukraine hadi itakapofanikisha malengo yake


Rais wa Russia Vladimir Putin
Rais wa Russia Vladimir Putin

Rais wa Russia Vladimir Putin amesema Alhamisi kwamba Amani itarejea  nchini Ukraine pale taifa lake litakapofanikisha  malengo yake, na azma hiyo haijabadilika.

Ikiwa imebaki miezi miwili kabla ya kuingia mwaka wa pili tangu uvamizi kamili wa Russia nchini Ukraine, Putin amesisitiza kwamba Russia inalenga kuhakikisha kumalizwa kwa misimamo ya ki Nazi, kuondolewa kwa silaha, pamoja na msimamo usioegemea upande wowote wa Ukraine, wakati alipokuwa akiongea na wana habari ikiwa ni mkutano wake wa mwisho wa mwaka.

Russia imerejea kusema kwamba serikali ya Ukraine ina ushawishi mkubwa wa makundi yenye misimamo mikali yakiwemo ya Nazi, madai ambayo Ukraine na washirika wake wa magharibi wameyapuuza na kusema hayana msingi kufanya uvamizi. Putin pia amesema kwamba Ukraine kamwe isijunge na NATO. Muungano huo hata hivyo umerudia mara kadhaa kusema kwamba ni jukumu la mataifa binafsi na siyo Russia.

Forum

XS
SM
MD
LG