Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 06:06

Polisi Uganda waokoa watoto 24 wakipatiwa mafunzo ya vita


Polisi nchini Uganda iliwaokoa watoto 24 kutoka kwenye kambi inayoaminika kuwa ya mafunzo ya kijeshi ya waasi wa kundi la Allied Democratic Forces-ADF, la nchini Uganda.

Watoto hao inasemekana kuwa wana umri kati ya miaka 2 na 15, na polisi walisema wana ushahidi wa video kuthibithisha kwamba watoto wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya vita.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:56 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Taarifa zaidi zinasema kwamba watoto walivalishwa mavazi ya ki-Islam ya Hijab, Taribush na Kanzu kwenye makazi yao yaliyopo Mpoma katika wilaya ya Mkono iliyopo nje kidogo ya jiji la kampala eneo la mashariki mwa Uganda.

Msemaji wa polisi nchini Uganda, Fred Enanga anasema kuna ushahidi wa picha za video zinazoonyesha watoto hao wakipatiwa mafunzo yanayoaminika kufanywa na kundi la waasi la ADF la nchini Uganda. “tulifanikiwa kuwaokoa watoto wachanga waliokuwa wakiishi maisha ya kuhuzunisha, malezi mabovu katika mazingira machafu n ahata kulishwa vibaya”.

Wakati huo huo waalimu wa watoto hao waliotambulika kwa majina ya Athuman Naluwoga na Abdurashid Mbazira walikamatwa na wanaripotiwa kuwa ni wanachama wa kundi la uasi la ADF. Mafunzo yalikuwa yakitolewa kwenye nyumba mbili zilizojengwa kwa matope zilizokuwa zikitumika kama madarasa na mabweni kwa wavulana 12 na wasichana 12.

Polisi nchini Uganda hivi sasa inawatafuta wazazi wa watoto hao.

XS
SM
MD
LG