Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:21

Papa Francis atoa msaada wa $121,000 kwa waathiriwa wa mashambulizi Msumbiji


Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis (Kushoto)
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis (Kushoto)

Kiongozi mkuu wa kanisa Papa Francis ametoa msaada wa dola za Marekani 121,000 kwa waathiriwa wa mashambulizi ya wanamgambo katika jimbo la kaskazini mwa Msumbiji la Cabo Delgado.  

Hii ni kufuatia wito uliotolewa na askofu wa Pemba Luis Fernado Lisboa, kutaka msaada kwa maelfu ya watu waliofurushwa makwao na wavamizi wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislamu.

Wanamgambo hao wamekuwa wakifanya mashambulizi katika eneo hilo tangu mwaka wa 2017 na takriban watu 430,000 wamebaki bila makazi.

Askofu Liboa aliwaambia waandishi wa habari Jumatatu kwamba msaada huo, utatumiwa kujenga vitoa vya afya, hususan katika maeneo ambako wakimbizi wengi wanahifadhiwa, katika wilaya za Montepuez na Chiure.

XS
SM
MD
LG