Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 16, 2025 Local time: 12:21

Pakistan yafungua tena mpaka wake na Afghanistan


Foleni ndefu za magari kwenye mpaka wa Torkham kati ya Pakistan na Afghanistan muda mfupi baada ya kufungwa hapo awali.
Foleni ndefu za magari kwenye mpaka wa Torkham kati ya Pakistan na Afghanistan muda mfupi baada ya kufungwa hapo awali.

Pakistan Ijumaa imefungua mpaka wa Torkham na taifa jirani la Afghanistan lisilo na bandari, baada ya kufungwa kwa siku 9 kufuatia hofu ya mashambilizi ya kigaidi pamoja na masuala mengine ya kiusalama, kulingana na maafisa kutoka mataifa yote mawili.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya waziri wa mambo ya kigeni wa Taliban Amir Khan Muttaqi, kuahidi wakati wa mkutano wa Alhamisi kati yake na kaimu balozi wa Islamabad mjini Kabul, kwamba utawala wa Taliban hautaruhusu visa vya kigaidi dhidi ya Pakistan kufanyikia kwenye mchanga wa Afghanistan.

Hayo ni kwa mujibu wa afisa wa Pakistan aliyezungumza na VOA kwa masharti ya kutotambulishwa kwa kuwa hajaruhusiwa kuzungumza moja kwa moja na vyombo vya habari. Afisa wa mpakani wa Pakistan amedhibitisha kwamba wafanyakazi wa uhamiaji na usalama wameagizwa warejee kwenye ofisi zao zilizopo kwenye mpaka huo.

Forum

XS
SM
MD
LG