Taarifa hiyo ya Oktoba 10, inashutumu Umoja wa Mataifa kwa kutumia mbinu za kijanja zilizochochewa na Ufaransa kuzuia ushiriki kamili wa Niger kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja huo mwezi uliopita pamoja na na mikutano mingine ya kimataifa. Utawala wa kijeshi ulimuondoa madarakani rais aliyechaguliwa kidemokrasia mwezi Julai, pia umevifukuza vikosi vya Ufaransa pamoja na balozi wake nchini humo.
Forum