Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Januari 19, 2025 Local time: 07:38

Niger imeanza kuendesha mtambo wake wa umeme wa jua; Anasema waziri wa nishati


Mji wa Tillaberi uliopo nchini Niger
Mji wa Tillaberi uliopo nchini Niger

Mahaman Moustapha Barke, amesema kupitia televisheni kuwa kampuni ya kitaifa ya umeme ya Nigelec tayari imeeleza “kuboresha ubora wa huduma” katika mji mkuu Niamey na miji ya Dosso na Tillaberi

Niger imeanza kuendesha mtambo wake mkubwa wa umeme wa jua, waziri wa nishati alisema Jumapili, akielezea uhaba wa umeme baada ya nchi jirani ya Nigeria a kuacha kupeleka vifaa vya umeme kufuatia vikwazo kutokana na mapinduzi ya Julai.

Mahaman Moustapha Barke, amesema kupitia televisheni kuwa kampuni ya kitaifa ya umeme ya Nigelec tayari imeeleza “kuboresha ubora wa huduma” katika mji mkuu Niamey na miji ya Dosso na Tillaberi.

Nishati ya jua inapatikana kwa wingi katika nchi isiyo na bandari taifa la Afrika Magharibi ambalo sehemu kubwa ni jangwa. Kituo hicho kina vifaa vya umeme wa jua zaidi ya 55,000 na kina uwezo wa kuzalisha megawati 30 za umeme.

Kilitarajiwa kufanya kazi kuanzia Agosti 25 lakini kuanza kwa shughuli hiyo kulicheleweshwa baada ya wafanyakazi wengi wa kiufundi kuondoka kufuatia mapinduzi hayo, Barke aliongeza.

Forum

XS
SM
MD
LG