Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 06:27

New Zealand yaondoa kanuni zote za Covid


Waziri mkuu wa New Zealand Chris Hipkins wakati akitangaza kumalizika kwa kanuni za Covid bungeni mjini Wellington, Aug. 14, 2023.
Waziri mkuu wa New Zealand Chris Hipkins wakati akitangaza kumalizika kwa kanuni za Covid bungeni mjini Wellington, Aug. 14, 2023.

New Zealand Jumatatu imeondoa kanuni za mwisho zilikokuwa zimewekwa za kuzuia maambukizi ya Covid ,ikiwa hatua ya mwisho ya kurejea kwenye hali ya kawaida baada ya janga hilo ambalo lilifuatiliwa kwa kina kote ulimwenguni.

Waziri mkuu wa New Zealand Chris Hipkins amesema kwamba kanuni za kuvaa barakoa kwenye hospitali pamoja na maeneo mengine ya afya zitaondolewa usiku wa manane, zikiwemo zile pia zilizohitaji mtu aliyeambukizwa kujiweka karantini kwa siku 7. Mwanzoni New Zealand ilisifiwa kimataifa kutokana na kuangamiza kabisa kirusi hicho, kufuatia kufungwa kwa shughuli za kawaida kote nchini pamoja na kuweka sheria kali za usafiri kwenye mipaka. Hata hivyo kadri janga lilivyoendelea kuenea, pamoja na kujitokeza kwa aina tofauti za virusi , taifa hilo lililegeza baadhi ya juhudi zake baada ya kugundua kuwa hazikuwa zikifanya kazi.

Forum

XS
SM
MD
LG