Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 08:40

Netanyahu: 'Bora kuikabili Iran mapema...'


Waziri Mkuu wa Israeli akiongelea juu ya programu ya nyuklia ya Iran, huko Tel Aviv, Jumatatu, Aprili 30, 2018.
Waziri Mkuu wa Israeli akiongelea juu ya programu ya nyuklia ya Iran, huko Tel Aviv, Jumatatu, Aprili 30, 2018.

Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema kuwa Iran inawapa Syria silaha zenye ubora zaidi ambazo nitishio kwa Israel ni vyema kuikabili Tehran hivi sasa kuliko hapo baadae.

Netanyaju ameliambia Bunge la nchi hiyo linalokutana Jumapili kuwa “Tunadhamira ya kuzuia vitendo vya uchokozi vya Iran dhidi yetu hata kama hilo litakuwa kwa njia ya mapambano. Ni bora hilo lifanyike hivi sasa kuliko hapo baadae.” Aliongeza: Hatutaki kuongeza mvutano, lakini tuko tayari kwa hali yoyote.”

Israel imerudia mara kadha kuonya kuwa haiwezi kuvumilia uwepo wa kudumu wa majeshi ya Iran katika nchi jirani ya Syria.

Iran ni mshirika muhimu wa Rais wa Syria Bashar Assad, na imekuwa ikitoa misaada muhimu ya kijeshi kwa majeshi ya Assad.

XS
SM
MD
LG