Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 25, 2025 Local time: 11:34

Mwandishi wa habari aliyefungwa jela wakati wa maandamano aachiliwa huru


Mwanahabari Nazila Maroufian akionyesha ishara ya ushindi baada ya kuachiliwa jela Aug. 13, 2023.
Mwanahabari Nazila Maroufian akionyesha ishara ya ushindi baada ya kuachiliwa jela Aug. 13, 2023.

Mwandishi wa habari  wa Iran aliyehukumiwa  kifungo cha miaka 2 jela baada ya kumhoji baba wa msichana aliyekufa akiwa kwenye kizuizi cha polisi na kupelekea maandamano makubwa kwa miezi kadhaa kote nchini humo, amesema Jumapili kwamba ameachiliwa kutoka gerezani.

Muda mfupi baada ya kuachiliwa kwa mwanahari huyo Nazila Maroufian kutoka kwenye jela ya Evin mjini Tehran aliweka ujumbe kwenye mtandao wa X pamoja na Instagram ukiwa na picha yake akishikilia maua mkono mmoja huku akiunyoosha mkono mwingine na kuonyesha ishara ya ushindi.

Maroufian ambaye umri wake ulitajwa kuwa miaka 23 na chombo kimoja cha habari cha Uajemi, Oktoba mwaka uliopita, alifanya mahojiano kwenye jukwa la mtandao la Mostaghel na Amjad Amini ambaye ni baba yake Mahsa Amini ambaye alifia jela baada ya kukamatwa kwa madai ya kukiuka kanuni ya kuvaa hijab, na kupelekea maandamano makubwa Septemba mwaka jana kote nchini Iran.

Forum

XS
SM
MD
LG