Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 18:05

Museveni ayataka mataifa ya Afrika yajitoe ICC


Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameyataka mataifa ya Afrika kujitoa katika mkataba unaounda mahakama ya kimataifa ya uhalifu – ICC, kwa kile anachodai kuwa taasisi hiyo ya kimataifa inawalenga waafrika isivyo haki.

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameyataka mataifa ya Afrika kujitoa katika mkataba unaounda mahakama ya kimataifa ya uhalifu – ICC, kwa kile anachodai kuwa taasisi hiyo ya kimataifa inawalenga waafrika isivyo haki.

Akiongea katika kilele cha maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa kenya zilziofanyika mjini Nairobi, Rais Museveni amesema atawasilisha mswaada katika kikao kijacho cha Umoja wa Afrika ili mataifa yote wanachama wa au yajiondoe katika mkataba huo wa ICC na kuwaachia magharibi wabakie humo.

Akizungumza kwa hamasa rais Museveni amesema awali alikuwa akiiunga mkono ICC kwa vile anaheshimu nidhamu na kutaka kila mmoja awajibishwe kwa makosa yake, lakini taasisi hiyo imegeuka ni chombo cha kuikandamiza afrika na kusema kwa maneno sitafanya kazi nao tena.

Waendesha mashtaka wa icc hivi karibuni walimfutia mashtaka Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta lakini naibu wake bado anaendelea kukabiliwa na mashtaka katika mahakama hiyo.

XS
SM
MD
LG