Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 07:46

Museveni asema hataruhusu maandamano.


Rais wa Uganda Yoweri Museveni alipokula kiapo.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni alipokula kiapo.

Rais Yoweri Museveni apinga maandamano nchini Uganda baada ya wiki kadhaa za maandamano.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema hataruhusu maandamano nchini humo kuendelea baada ya wiki kadhaa za maandamano dhidi ya serikali.

Bw. Museveni alisema hayo katika taarifa ya maandishi jumanne kwamba atatumia kila kipengele cha sheria kumaliza kile alichokiita uhalifu huu. Aliwalaumu polisi na mahakama kuwa wapole mno na kusema kwamba kuna udhaifu katika sheria ambayo inaruhusu utovu wa nidhamu kuwepo.

Rais huyo pia alishutumu vyombo vya habari vya nyumbani na vya kimataifa kwa kushangilia kile alichokiita watu wasio makini ambao ni maadui wa mafanikio ya uponyaji ya Uganda.

XS
SM
MD
LG